Posts

TRC YAANZA RASMI USAFIRISHAJI WA MIZIGO KWA KUTUMIA CONTAINER CARRIERS SGR.

Image
Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanza rasmi usafirishaji wa makasha kwa kutumia reli ya Standard Gauge, hatua inayolenga kupanua wigo wa biashara, kupunguza msongamano wa mizigo bandarini na kurahisisha usafirishaji wa mizigo kwenda mikoa ya kati ya nchi. Akizungumza wakati wa kuanza safari ya treni ya kwanza ya makasha kutoka Pugu kuelekea Ihumwa mkoani Dodoma, Kaimu Mkurugenzi wa Usafirishaji wa TRC, Focus Makoye Sahani, amesema treni hiyo inasafiri umbali wa takribani kilometa 420 kutoka Dar es Salaam. Amesema hatua hiyo ni mwanzo wa usafirishaji wa makasha baada ya TRC kuanza kusafirisha abiria pamoja na mizigo mbalimbali ikiwemo kichele kuanzia mwezi Julai, pamoja na saruji inayopakiwa Pugu. “Leo tumeongeza wigo wa biashara kwa kupakia makasha. Kama mnavyoona, treni yetu ya kwanza ya makasha kwenda Ihumwa, Dodoma, leo imeanza safari zake na tuna ofa ya kutosha kutoka kwa mteja wetu wa kwanza,” amesema Sahani. Ameeleza kuwa treni hiyo ina mabehewa 50 yanayobeba jumla ya makasha 1...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

WAZIRI NDEJEMBI AKABIDHI MAGARI KWA MAMENEJA WA TANESCO - TABORA

Image
Waziri wa nishati Mhe. Deogratius Ndejembi amekabidhi vitendea kazi vya usafiri kwa mameneja wa TANESCO wa Wilaya za Skonge, Urambo na Igunga Mkoani Tabora  ili kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi na kutatua changamoto zao kwa wakati. Akizungumza wakati akikabidhi magari hayo kwa Meneja wa TANESCO wilayani Urambo kwa niaba ya wengine, Mhe. Ndejembi amempongeza Mkurugenzi Mtendaji Bw. Lazaro Twange kwa kuchukua hatua za haraka kwa ajili ya kuhakikisha mwananchi anafikiwa bila kujali mazingira aliyopo. Amesema hatua hiyo  ya kununua vitendea kazi ni kuyaishi maono ya Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan juu ya utendaji kazi katika Mashirika ya umma ambapo TANESCO imeonesha mfano na sasa wateja takribani milioni 5.6 watapata umeme wa uhakika na kuhudumiwa kwa wakati.  ‘’Ninatamani kuona mnafanya mabadiliko makubwa katika kumfikia mteja kwa haraka, eneo la kumsikiliza na kumuhudumia mteja tunafanya vizuri sana, sasa tukaongeze nguvu ya kutatua changamoto za wateja kwa wakati k...

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 70 ZIMEKUSANYWA KUPITIA MRADI WA EACOP- MHE.SALOME

Image
Serikali imekusanya zaidi ya shilingi bilioni 70 kupitia tozo, ada na ushuru mbalimbali zitokanazo na utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), na inatarajia kukusanya zaidi ya shilingi trilioni 2.3 mradi utakapoanza kuingia katika hatua ya uendeshaji. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema hayo tarehe 16 Februari 2026 wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika mradi wa EACOP mkoani Tanga. Mhe. Salome amesema mradi huo ambao umefikia asilimia 81  ulianza kutekelezwa mwaka 2022 na unahusisha ujenzi wa bomba lenye urefu wa kilomita 1,443 pamoja na miundombinu mingine ikiwemo matenki na gati la kupakia mafuta. Amefafanua kuwa mradi unatekelezwa kwa gharama ya dola za Marekani bilioni 5.649, huku Serikali ya Tanzania ikichangia dola milioni 374 sawa na asilimia 15 ya hisa. Katika sekta ya ajira, amesema mradi umezalisha jumla ya ajira 10,000 katika kipindi cha ujenzi, ambapo asilimia 75 sawa na ajira 7,500 zimenufaish...

RC CHALAMILA AZINDUA UTOAJI HUDUMA ZA SHERIA BURE KWA WANANCHI.

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Feb 16,2026 amezindua rasmi utoaji wa huduma bure za kisheria kwa wananchi wa Mkoa huo na Mikoa jirani katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam chini ya uratibu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. RC Chalamila akizindua huduma hiyo amesema kuwepo kwa huduma bure ya kisheria kutasaidia kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali, malalamiko ya kisheria kutoka kwa wananchi, vitendo vya uonevu vinavyovunja sheria na taratibu pia kwa kuwa kuna kamati za mashauri ya kisheria nazo zitatoa elimu ya sheria kwa umma katika kushughulikia changamoto mbalimbali katika maeneo yao. Aidha RC Chalamila amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassani kupitia ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuandaa klinik hiyo ambayo inatimu ya Mawakili wabobevu ambao watakuwa wanatoa huduma za kisheria bila malipo kwa wananchi wote watakaohudhuria katika viwanja hivyo kwa wananchi wote wa Mkoa wa Dar ...

TUTATENGA FEDHA ZA KUJENGA BARABARA YA KUELEKEA KAMPASI YA MZUMBE TANGA- PROF. SHEMDOE.

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaahidi wananchi wa Mkinga kuwa katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha  2026/27 kupitia TARURA itatengwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa   barabara yenye urefu wa kilomita 16 kwa kiwango cha changarawe, ambazo zitaunganisha Chuo cha Mzumbe Kampasi ya Tanga na barabara kuu ya TANROADS ili kuwezesha kampasi hiyo kufikika kwa urahisi. Prof. Shemdoe ametoa ahadi hiyo leo Februari 15, 2026 baada ya Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Mchemba, kumtaka Prof. Shemdoe kueleza mkakati wa kutatua changamoto ya ubovu wa barabara hiyo iliyowasilishwa na Mbunge wa Mkinga Mhe. Twaha Said Mwakioja na uongozi wa chuo, wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika Chuo Kikuu cha Mzumbe Kampasi ya Tanga. "Mhe Waziri Mkuu ili kufika hapa Kampasi ya Chuo Kikuu cha Mzumbe kuna umbali wa kilomita 16 zinazoangukia TARURA kutoka ilipo barabara kuu ya TANROADS, katika bajeti mwaka wa fedha 2026/27 tutatenga fedha ya kujenga barabara hii...

KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TCPM – TABORA CHA SERIKALI SIO TISHIO KWA SEKTA BINAFSI: NDEJEMBI

Image
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema ujenzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Nguzo za Zege cha TCPM Tabora kinachomilikiwa na Shirika la Umeme Tanzania - TANESCO kupitia kampuni tanzu ya TCPM haukusudii kuathiri wala kudhoofisha uwekezaji wa sekta binafsi bali unaongeza uzalishaji wa nguzo za zege ili kukidhi mahitaji yaliyopo ambayo bado hayajatosheleza uhitaji wa nguzo hizo nchini. Ameeleza hayo Februari 15, 2026 wakati akikagua mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Nguzo za Zege cha TCPM Tabora, ambao umefikia asilimia 95 ya utekelezaji. Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha wastani wa nguzo za zege 120 kwa siku. “Kiwanda hiki si tishio kwa sekta binafsi; kinakuja kuongeza nguvu katika kazi ambazo tayari zilikuwa zinafanywa na sekta binafsi ya kuzalisha nguzo za zege,” amesema Ndejembi. Ndejembi amefafanua kuwa TANESCO kwa mwaka 2025 ilikuwa na uhitaji wa nguzo za zege 80,000, lakini zilizopatikana kupitia sekta binafsi ni nguzo 40,000 jambo lililosababisha kuto...