Cairo, Misri, Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi leo Juni 8, 2026 ameshiriki Ufunguzi wa Jukwaa la Utalii, Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Misri linalofanyika jijini Cairo, likiwakutanisha viongozi wa Serikali, taasisi za utalii, wafanyabiashara, wawekezaji na wadau mbalimbali kutoka nchi hizo mbili kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kukuza fursa za biashara, uwekezaji na utalii. Jukwaa hilo limeandaliwa chini ya kaulimbiu inayohamasisha uhusiano kati ya Bahari ya Mediterania na Bahari ya Hindi kupitia masoko, utalii, biashara na uwekezaji, likitoa fursa kwa wadau kujadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano yenye manufaa kwa pande zote mbili. Katika jukwaa hilo, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imeshiriki mjadala ambapo washiriki walijadili fursa za ushirikiano katika sekta za utalii, biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Misri. Aidha, washiriki walipata fursa ya kushuhudia video mbalimbali za kutangaza...