Posts

BARAZA JIPYA LA NIT LATAKIWA KUIMARISHA TAFITI NA MAFUNZO YA UCHUKUZI

Image
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, ameliagiza Baraza la 13 la Uongozi la National Institute of Transport kuhakikisha linasimamia kwa ufanisi mafunzo na tafiti zinazolenga kutatua changamoto za sekta ya usafirishaji na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Akizindua baraza hilo mkoani Morogoro, Prof. Mbarawa amesema chuo kina wajibu mkubwa wa kuisaidia Serikali katika kuandaa sera na mikakati madhubuti ya maendeleo ya sekta ya uchukuzi nchini. Amesema utekelezaji wa jukumu hilo utawezesha chuo kufikia malengo ya mpango wake wa miaka mitano unaolenga kuboresha ubora wa elimu na mafunzo, kukidhi mahitaji ya soko la ajira la kisasa pamoja na kuimarisha miundombinu ya kujifunzia ikiwemo maabara, maktaba na matumizi ya teknolojia za kisasa. Prof. Mbarawa ameongeza kuwa maandalizi ya awali ya Sera Mpya ya Taifa ya Uchukuzi yameanza kuzingatia mifumo mipya ya usafiri kama Cable Transport na Space Transport, hivyo akalitaka baraza hilo kuandaa wataalamu watakaoweza kuhudumia maeneo ...

MAMIA YA WATANZANIA TABORA KUNUFAIKA NA UPASUAJI WA MTOTO WA JICHO BILA MALIPO

Image
Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya afya, ikiwemo Helen Keller International, imeanzisha kambi maalum ya uchunguzi na upasuaji wa mtoto wa jicho katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, ambapo takribani wananchi 700 wanatarajiwa kunufaika na huduma hizo bila malipo. Miongoni mwa wanufaika ni Henry Machibya (62), mkazi wa Simbo wilayani Igunga, ambaye amesema tatizo la macho lilianza mwaka 2023 na kuendelea kuathiri uwezo wake wa kuona hadi kupoteza kabisa uwezo wa kuona kwa macho yote mawili katika miezi ya hivi karibuni. Machibya amesema hali hiyo ilimlazimu kuacha shughuli zake za kilimo ambazo zilikuwa chanzo chake kikuu cha mapato na kujikuta akitegemea msaada wa watu wa karibu katika kutekeleza mahitaji ya msingi ya kila siku. “Nilikuwa nikitegemea kilimo kwa ajili ya kujikimu na kuhudumia familia yangu, lakini hali ya macho yangu ilibadilisha maisha yangu kabisa,” amesema. Aidha, amesema changamoto nyingine alizokumbana nazo n...

KILLOLO DC YAVUTIA UTALII IKOLIJIA KILOMBERO, DAS BI. NYAKAJI AONGOZA KAMBI CHUI CAMPSITE.

Image
Kilombero Nature Reserve, Iringa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kilolo, ikiongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Bi. Nyakaji Etanga, imehimiza wananchi na watumishi wa umma kutumia fursa za utalii ikolojia zilizopo ndani ya Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Kilombero (Kilombero Nature Forest Reserve), baada ya kufanya ziara na kupiga kambi katika kituo cha utalii cha Chui Campsite kilichopo Udekwa. Ziara hiyo iliyofanyika kuanzia Juni 3 hadi Juni 4, 2026 ilihusisha viongozi wa kamati hiyo waliopata fursa ya kufanya kambi ndani ya hifadhi, hatua iliyolenga kuhamasisha utalii wa ndani na kuongeza uelewa wa uhifadhi wa mazingira kupitia uzoefu wa moja kwa moja wa vivutio vilivyopo. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bi. Nyakaji Etanga alisema ameridhishwa na mandhari ya kipekee ya Chui Campsite pamoja na fursa mbalimbali za kiutalii zilizopo ndani ya hifadhi hiyo, akisisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika utalii ikolojia kama njia ya kuchochea maendeleo ya kiuch...

Serikali Kupeleka Umeme Katika Mitaa 14 Iliyosalia Tarime Mjini

Image
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imepanga kupeleka umeme katika mitaa 14 iliyosalia bila huduma hiyo katika Mji wa Tarime, kwa kuhakikisha mitaa yote inafikiwa na umeme. Mhe. Salome amesema hayo leo, Juni 8, 2026, Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mhe. Ester Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini, aliyetaka kujua ni lini umeme utafika katika mitaa yote isiyo na umeme katika Mji wa Tarime. Amesema Mji wa Tarime una jumla ya mitaa 81, ambapo mitaa 54 ina umeme na mitaa 27 haina umeme. Amefafanua kuwa kati ya mitaa 27 isiyo na umeme, mkandarasi anaendelea na kazi katika mitaa 13 na hadi sasa ameshasimamisha nguzo huku akijiandaa kuanza kufunga nyaya. Aidha, Mhe. Salome amesema Serikali kupitia TANESCO imepanga kupeleka umeme katika mitaa iliyosalia kulingana na upatikanaji wa fedha, kwa lengo la kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 kila mtaa nchini umefikiwa na huduma ya umeme. Kadhalika, Mhe. Salome ametumia nafasi...

TANZANIA YASHIRIKI JUKWAA LA UTALII, BIASHARA NA UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA MISRI

Image
Cairo, Misri, Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi leo Juni 8, 2026 ameshiriki Ufunguzi wa Jukwaa la Utalii, Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Misri linalofanyika jijini Cairo, likiwakutanisha viongozi wa Serikali, taasisi za utalii, wafanyabiashara, wawekezaji na wadau mbalimbali kutoka nchi hizo mbili kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kukuza fursa za biashara, uwekezaji na utalii. Jukwaa hilo limeandaliwa chini ya kaulimbiu inayohamasisha uhusiano kati ya Bahari ya Mediterania na Bahari ya Hindi kupitia masoko, utalii, biashara na uwekezaji, likitoa fursa kwa wadau kujadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano yenye manufaa kwa pande zote mbili. Katika jukwaa hilo, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imeshiriki mjadala ambapo washiriki walijadili fursa za ushirikiano katika sekta za utalii, biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Misri.  Aidha, washiriki walipata fursa ya kushuhudia video mbalimbali za kutangaza...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image