Posts

Showing posts from January, 2026

Naibu meya John Ryoba Mrema afungua Barabara Kinyerezi .

Image
Na Heri Shaaban( Dar es Salaam) NAIBU MEYA wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam John Ryoba Mrema afungua Barabara za mitaa ndani ya kata ya Kinyerezi Wilaya ya Ilala   Naibu meya John Ryoba Mrema amefungua Barabara hizo Dar es Salaam leo katika mitaa yote ya kata ya Kinyerezi kwenye changamoto awali wananchi wake walikuwa wakipata shida katika huduma mbalimbali za usafiri . "Mimi ni Diwani wa kata ya Kinyerezi awali wakati naomba kura kuwatumikia wananchi nilieleza nitakapoingia madarakani nitatatua changamoto mbalimbali katika utekelezaji wa Ilani ya chama kwa sasa nimeanza na miundombinu ya Barabara "alisema John Ryoba.  Diwani Ryoba Mrema alisema kwa sasa barabara hizo za ndani  zote zitaanza kupitika  ukarabati umeanza sambamba na kuweka vifusi  na karavati.  Alisema awali Barabara hizo zilikuwa changamoto kina Mama Wajawazito kuzitumia kwa sasa mara baada kumalizika ukarabati zitatumika zote kwa huduma mbalimbali . Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Sha...

RC CHALAMILA "VIMBA NA IST FEBRUARI 14,2026.

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amewatangazia wakazi wa Mkoa huo hususani vijana kushiriki Tamasha la IST Festival linalotarajia kufanyika februari 14 mwaka huu kwenye viwanja vya Coco beach ikiwa ni katika kuunganisha wananchi na kuimarisha umoja,upendo na mshikamano baina ya yao. Akizungumza katika viwanja vya Coco beach na waandishi wa habari Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amesema anatambua kuwa hivi karibuni wananchi wametoka kwenye uchaguzi na wameingia mwaka mpya 2026 hivyo kupitia tamasha hilo itasaidia kuwaunganisha wananchi kuwa pamoja, kusherekea, pia kupeana  fursa mbalimbali pamoja na zawadi ikiwemo magari aina ya IST kwa watakaoshiriki vyema. Aidha RC Chalamila amesema kupitia Tamasha hilo wananchi watapata fursa ya kupima na kujua afya zao hususani kwenye changamoto za maradhi ya moyo ambapo Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete inatarajia kushiriki kwa kutoa huduma za upimaji afya. Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Nurdeen Bilali ...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

RAIS DKT. MWINYI: SMZ YAENDELEA KUIMARISHA MAZINGIRA BORA YA UWEKEZAJI ZANZIBAR.

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewahakikishia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwa Serikali itaendelea kuweka vivutio na mazingira bora ya uwekezaji kwa lengo la kunufaika na miradi yao. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 20 Januari 2026, wakati wa uzinduzi wa boti mpya ya Kilimanjaro 9 (Dragon of the Sea) inayomilikiwa na Kampuni ya Azam Marine Ltd, katika hafla iliyofanyika Mtoni Verde, Mkoa wa Mjini Magharibi. Amesema Serikali inaendelea kuimarisha sekta ya usafirishaji baharini kupitia ujenzi wa miundombinu ya bandari ikiwemo Bandari ya Fumba na bandari nyingine Unguja na Pemba, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi na kuboresha huduma za usafiri baharini. Rais Dkt. Mwinyi amempongeza Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam, Mzee Said Salim Bakhresa, kwa uwekezaji mkubwa unaogusa maisha ya wananchi, akibainisha kuwa kampuni hiyo imewekeza Dola za Marekani Milioni 150 na kutoa ajira 281. Kwa upande wake, Mtendaji...

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA: KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KASI YA WIZARA YA NISHATI.

Image
Na Mwandishi Wetu, Dodoma Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Nishati kwa kazi kubwa inayoendelea kutekelezwa ndani ya siku 100 za uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwemo kuanza kusambaza umeme katika vitongoji 9,009, hatua inayoonesha mwelekeo chanya wa utendaji wa kipindi cha pili cha Serikali ya Awamu ya Sita. Pongezi hizo zimetolewa Januari 20, 2026 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wizara ya Nishati, taasisi zilizo chini yake pamoja na Kamati hiyo.  Kikao hicho kimelenga kuijengea Kamati uelewa kuhusu muundo na majukumu ya Wizara ya Nishati, pamoja na sera na sheria mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara hiyo katika kuendeleza Sekta ya Nishati nchini. Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mgalu amesema mafanikio yaliyopatikana ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Samia ni ushahidi wa dhamira ya Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa wananchi....

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

MKURUGENZI MKUU REA AWAFUNDA WAHANDISI WA MIKOA.

Image
Dodoma  Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewaelekeza Wasimamizi wa Miradi wa Mikoa kuhakikisha wanaimarisha Mawasiliano na Ushirikiano na wadau mbalimbali kwenye maeneo ya miradi ili kurahisisha utekelezaji wake.  Ametoa maelekezo hayo leo Januari 19, 2026 jijini Dodoma katika kikao chake na Watumishi wa REA wanaohusika na Usimamizi wa Miradi wa Mikoa mara baada ya Kusaini mikataba ya kusambaza umeme katika Vitongoji 9,009 Tanzania Bara. "Tarehe 17 Januari, 2026 tulisaini mikataba na Wakandarasi ya kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 na tunaelekea kwenye hatua ya utekelezaji, nimewaiteni hapa ili tukumbushane namna bora ya kuimarisha utendajikazi wetu," amesisitiza Mha. Saidy. Amesema Watanzania wanayo matumaini na REA na kwamba ni wajibu wao kuhakikisha hawawaangushi kwa kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Taratibu na Miongozo ya Serikali. "Imarisheni mawasiliano na ushirikiano na Wabunge, Viongozi wa Mikoa, Wilaya, TANESCO, Wak...

DC KIBAHA AUPA MSUKUMO UVUNAJI ENDELEVU MISITUNI.

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, amezitaka serikali za vijiji wilayani humo kuwa mstari wa mbele katika kulinda rasilimali za misitu kwa kuhakikisha mpango wa uvunaji endelevu wa mazao ya misitu unatekelezwa kikamilifu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Mhe. Simon alitoa msisitizo huo leo Januari 19, 2026, wakati wa Kikao cha Tathmini ya Nusu Mwaka (Julai–Desemba 2025) kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikoko, ofisi za Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki, wilayani Kibaha, mkoani Pwani. Alisema vijiji vina jukumu la kutoa taarifa mara moja pale uvunaji unapobainika kufanyika kinyume cha taratibu, pamoja na kuwasilisha taarifa za wavunaji wanaokiuka sheria mara kwa mara, ili mamlaka zichukue hatua stahiki kwa mujibu wa sheria. Katika kuimarisha usimamizi wa misitu, Mhe. Simon aliagiza asilimia 20 ya mapato yote yanayokusanywa ngazi ya kijiji itengwe kwa ajili ya kusimamia upandaji wa miti inayotolewa na TFS, akisisitiza umuhimu wa kuit...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

PROF. SHEMDOE AKEMEA TABIA YA WANANCHI KUTUPA TAKATAKA KWENYE BARABARA ZA MANISPAA YA MOROGORO.

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekemea tabia ya baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Morogoro kutupa takataka katika barabara za Muhimbili, Tubuyu II, Mjimwema, Barakuda na Kihonda-VETA zenye urefu wa Kilomita 12.85 ambazo zimejengwa na Serikali kupitia na Mradi wa TACTIC ikizingatiwa kuwa barabara hizo bado hazijakabidhiwa rasmi. Prof. Shemdoe amekemea kitendo hicho cha baadhi ya wananchi kutothamini miundombinu hiyo ya barabara, wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa mradi wa TACTIC katika Manispaa ya Morogoro. “Zimejengwa barabara nzuri sana lakini wananchi wenzangu mmeanza kutumia barabara hizi kama dampo la kutupa takataka, na si jambo jema kuendelea kutupa takataka wakati hatujakabidhiwa barabara,” amesisitiza Prof. Shemdoe.   Prof. Shemdoe amemtaka Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Khalid Matengo kutoa elimu kwa wananchi ya kuacha kutupa takataka katika miundombinu h...

REA YASAINI MIKATABA YA TRILIONI 1.2 YA KUSAMBAZA UMEME KATIKA VITONGOJI 9,009.

Image
Dodoma Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba 30 yenye thamani ya shilingi Trilioni 1.2 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme katika Vitongoji 9,009 utakaonufaisha Wateja wa awali 290,300  katika mikoa 25 ya Tanzania Bara. Akizungumza katika hafla hiyo leo, Januari 17, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kusaini kwa mikataba ya Mradi huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha ifikapo 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme. “Serikali imedhamiria kuhakikisha hakuna Mtanzania atakayebaki bila umeme. Tumekamilisha vijijini na sasa ni zamu ya vitongoji na kwa mikataba hii iliyosainiwa hivi leo ni ushahidi wa dhamira hiyo ya Serikali,” amesema Mhe. Ndejembi. Amebainisha kuwa kati ya mikataba 30 iliyosainiwa, mikataba 21 ni ya kampuni za Wazawa na mikataba mingine tisa ni ya kampuni kutoka Nje ya nchi ambazo zimesajiliwa hap...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

TANESCO KIGAMBONI YATOA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA SHULE YA MSINGI MALAIKA.

Image
Katika kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, TANESCO Mkoa wa Kigamboni ilitoa elimu ya matumizi ya umeme kwa ajili ya kupikia katika Shule ya Msingi Malaika iliyopo Kigamboni.  Elimu hiyo ilitolewa wakati wa siku maalum ya ufunguzi wa shule tarehe 13 Januari, 2026  (Back to School), iliyowakutanisha wazazi na walimu. Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO Mkoa wa Kigamboni, Bi. Tumaini Mahwaya, alisema kuwa lengo la kutumia fursa hiyo  ni kuhakikisha wazazi na waalimu wanapata uelewa wa kina kuhusu faida za kutumia nishati ya umeme kupikia akibainisha faida zake kuwa ni nishati salama, gharama nafuu na rafiki kwa mazingira. “Shirika linakenga kuhakikisha wazazi na walimu wanaelewa kuwa kupikia kwa umeme ni salama, ni nafuu na kunalinda afya pamoja na mazingira. Tukibadili mtazamo wetu leo, tutakuwa tumewekeza kwenye maisha bora ya baadaye,” alisema Tumaini. Vile vile, ili kuunga mkon...

BALOZI DKT EMMANUEL NCHIMBI KUZINDUA JENGO LA WAGENI MASHUHURI JNIA JANUARI 16

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi anatarajia kuzindua rasmi jengo la wageni mashuhuri katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Julias Nyerere jijini Dar es salaam Januari 16, 2026 Akizungumza Jijini Dar es salaam kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila  mbele ya waandishi wa habari Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakar Kunenge amesema jengo hilo lililojengwa kwa fedha za Serikali katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Julius Nyerere Terminal 1 limekamilika kwa asilimia miamoja na kwamba sasa lipo tayari kuzinduliwa rasmi hapo kesho RC Kunenge amesema jengo hilo litakua kwa ajili ya viongozi wa kitaifa,wakuu wa nchi mbalimbali wanaotembelea nchini Tanzania pamoja na wageni mashuhuri hivyo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya uzinduzi huo ambao utahudhuriwa ni viongozi mbalimbali. Aidha Kunenge amesema uwanja huo ni moja ya vichocheo vya ukuaji wa uchumi kwa nchi ya Tanzania na kwamba wakati wa ujenzi wa jengo h...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

WIZARA YA NISHATI KUSHIRIKIANA NA TBC KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

Image
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja  amepokea ujumbe rasmi kutoka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wenye lengo la kuimarisha ushirikiano katika kuitangaza Wizara ya nishati hususani katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini. Akizungumza leo Januari 15, 2026 Katika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma, baada ya kupokea ujumbe huo, Bi. Neema Mbuja alimshukuru Mkurugenzi wa Habari na Matukio Shirika la Utangazaji Tanzani (TBC), Bi. Eshe Muhidin pamoja na timu yake kwa kuendelea kuitangaza Wizara ya nishati pamoja na ajenda ya nishati safi ya kupikia kupitia Bongo FM na TBC kwa ujumla. “Tunashukuru sana juhudi za TBC katika kuelimisha jamii kuhusu nishati safi ya kupikia, kwani kupitia ushirikiano huu tunakusudia kuifanya ajenda hii isambae kwa upana zaidi na kuwafikia wananchi wengi zaidi ili kutimiza azma ya Mhe. Rais ya Kuhakikisha ifikapo 2034 asilimia 80% ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia” alisema Bi. ...

SERIKALI KUPITIA REA KUZINDUA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI.

Image
Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kuzindua Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Mtera na Kusaini Mikataba ya kutekeleza mradi kabambe wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 katika Mikoa yote Tanzania Bara. Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy amesema hayo Jijini Dodoma Januari 15, 2026 katika mkutano maalum na wanahabari  alipokuwa akitambulisha matukio hayo mawili yatakayoshuhudiwa na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ambaye atakuwa mgeni rasmi. “Tarehe 16 Januari, 2026 Kituo cha Kupoza Umeme cha Mtera kitazinduliwa rasmi na tarehe 17 Januari, 2026 tutasaini mikataba 30 yenye thamani ya shilingi Trilioni 1.2 kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji zaidi ya 9,000,” amefafanua Mha. Saidy Amebainisha kuwa Kituo cha Mtera kimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 9.2 na Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa ushirikiano na Serikali za Sweden na Norway. Aidha, Mhandisi Saidy amesema REA itasaini mikataba 30...

WAZIRI MKUU AKUTANA NA BALOZI WA JAPAN NCHINI.

Image
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yoichi Mikami na kujadiliana naye masuala ya uchumi, miradi ya maendeleo na uwekezaji. Akizungumza na Balozi huyo leo (Jumatano, Januari 14, 2026) ofisini kwake Mlimwa jijini Dodoma, Waziri Mkuu ameishukuru nchi hiyo kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania kukamilisha ujenzi wa miradi mbalimbali kama vile barabara ya Arusha hadi Holili, bandari ya Kigoma, miradi ya kilimo na upatikanaji wa vifaa tiba vya huduma za afya ya mama na mtoto. “Serikali itahakikisha kuwa miradi hii inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na inakamilishwa kama ilivyopangwa,” amesema Dkt. Mwigulu  Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kutuma salamu za pongezi kwa Waziri Mkuu wa Japan, Bibi Sanae Takaichi kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo tangu Oktoba, 2025 na kuweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo nchini humo. “Tanzania inasisitiza kuendeleza ushirikiano wa karibu na Japan kwa manufaa ya pande zote mbili,” amesema. ...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

KATAMBI, AYOUB WAPOKELEWA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

Image
Waziri wa Mambo ya Ndani Nchi, Mhe. Patrobas Katambi amekabidhiwa Ofisi na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mhe. George Simbachawene leo Januari 14, 2026, Ofisi za Wizara, Mtumba jijini Dodoma. Miongoni mwa Viongozi waliohudhuria halfa hiyo ni pamoja na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Ayoub Mohamed Mahmoud, Katibu Mkuu Ally Gugu, Naibu Katibu Mkuu Dkt. Maduhu Kazi, Wakuu wa Vyombo vya Usalama, Wakuu wa Idara na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

WAZIRI WA MASUALA YA JAMII DRC ATEMBELEA KAMBI YA WAKIMBIZI NYARUGUSU.

Image
Ujumbe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ukiongozwa na Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala ya Ustawi wa Jamii, Hatua za Kibinadamu na Mshikamano, Mhe. Eve Bazaiba Masudi, umetembelea Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu, mkoani Kigoma, kwa lengo la kujionea hali ya maisha ya wakimbizi na kusikiliza maoni pamoja na mapendekezo yao kwa Serikali ya DRC. Katika ziara hiyo, Mhe. Masudi aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kutoa hifadhi kwa wakimbizi kutoka DRC kwa takribani miaka 30 sasa, tangu kambi hiyo ilipoanzishwa. Amesema Tanzania imekuwa kisiwa cha amani na utu, na kwamba ukarimu huo umechangia kulinda hadhi ya watu waliolazimika kukimbia kutokana na changamoto mbalimbali nchini mwao. Aidha, Waziri huyo ameeleza kuwa Serikali ya DRC inaendelea na jitihada za kutafuta suluhisho la kudumu la kurejesha amani, ili wakimbizi waweze kurejea nchini mwao kwa hiari. Amehimizwa wakimbizi kuishi kwa nidhamu na kuzingatia maadili, ili kulinda heshima ya nchi yao na kuth...