Posts

Showing posts from April, 2025

MWALIMU ATAPELIWA SH, MIL 12,470 NA MGANGA WA TIBA.

Image
Mwalimu wa shule ya Sekondari Nyakabungo Edward Bihemo Mwenye umri wa miaka 43 Mkazi wa mtaa wa Nyamanoro Wilaya ya llemela Mkoani Mwanza ametapeliwa na mganga wa tiba asilia aliyejulikana Kwa jina la Edward Emmanuel kiasi Cha sh, Mil 12,470. Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Mwanza Wilbroad Mtafungwa ameeleza kuwa jeshi la polisi lilimkamata Edward Emmanuel miaka 38 na mmiliki wa nyumba ya kulala wageni Private Lodge Mkazi wa Nyamohongolo Wilaya llemela Kwa kosa la kujipatia pesa Kwa njia ya udanganyifu. Mtafungwa ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo April 18 Mwaka huu kujipatia fedha Kwa njia ya udanganyifu Kwa kumlaghai Edward Bihemo kupitia kazi yake ya uganga wa tiba asilia. Mtuhumiwa Edward Emmanuel alimweleza Edward Bihemo kuwa ana uwezo wa kuzalisha fedha Kwa njia ya miujiza ambapo mtuhumiwa alichukuwa fedha hizo na kuziweka katika begi lake na kumuamuru mhanga awe anazitolea sadaka mara Kwa mara ili ziweze kuongezeka. ...

NIMERIDHISHWA NA MAANDALIZI KUELEKEA SHEREHE ZA MEI MOSI-MAJALIWA

Image
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na Maandalizi kuelekea sherehe za siku ya wafanyakazi duniani zitakazofanyika kesho Mei mosi, 2025 kitaifa Mkoani Singida katika Uwanja wa Bombadia   Ameyasema hayo leo Jumatano (Aprili 30, 2025) alipopokea taarifa na kukagua maandalizi ya Maadhimisho ya Sherehe hizo. Mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mheshimiwa Majaliwa ameipongeza kamati inayoratibu sherehe hizo na kuwataka kuhakikisha wanakamilisha maeneo machache yaliyobaki ambayo yanahitaji maboresho.   Awali, akitoa taarifa ya maandalizi hayo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema maandalizi yamekamilika kwa kiasi kikubwa na wapo tayari kumpokea Rais Dkt. Samia kwa ajili ya sherehe hizo.

WAFUNGWA NA MAHABUSU KUSIKILIZA KESI KWA MAHAKAMA MTANDAO NI KWA SABABU ZA KIUSALAMA: BASHUNGWA.

Image
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema kuwa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania litaendelea kuwawezesha Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao wakiwa magerezani kupitia Mahakama Mtandao, hasa kunapokuwepo na viashiria vya matishio ya kiusalama, ili kudumisha amani na kulinda usalama wa raia na mali zao. Ameeleza kuwa mojawapo ya sababu ya kuendelea kutumia Mahakama Mtandao ni masuala ya kiusalama, ambapo hivi karibuni baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wametoa matamko yanayoashiria uvunjifu wa amani na usalama, hali iliyosababisha baadhi ya Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao kwa njia ya mtandao. Bashungwa ameyasema hayo leo, tarehe 30 Aprili 2025 jijini Dodoma, alipoambata na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), kukagua Makasha ya kisasa ya Mahakama Mtandao yanayowezesha usikilizaji wa mashauri kwa njia ya kiteknolojia katima Gereza la Isanga -Dodoma “Jeshi la Poli...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo.

Image
 

Steve Nyerere Atoa Wito kwa Viongozi wa Dini Kuepuka Siasa Katika Nyumba za Ibada.

Image
  Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steve Mengele maarufu kama Steve Nyerere, amewaasa viongozi wa dini kuhakikisha wanahimiza amani na upendo katika nyumba za ibada, badala ya kupandikiza chuki za kisiasa kwa waumini wao, ili kudumisha amani iliyopo nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Steve alisema kuwa viongozi wa dini wana wajibu mkubwa wa kuitunza amani ya taifa, hivyo wanapaswa kuepuka tabia ya kueneza chuki au kutoa hotuba zenye mwelekeo wa kisiasa mbele ya waumini. “Viongozi wa dini wanaoingiza siasa za uchochezi kwenye nyumba za ibada, ni vyema wakaweka wazi kwamba wameamua kuingia kwenye siasa, badala ya kuhubiri neno la Mungu. Wajiweke wazi tu, tutawaelewa,” alisema Steve. Aliongeza kuwa viongozi wa dini wanapaswa kubaki kwenye jukumu lao la kufundisha maadili mema kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Mambo ya kisiasa, alisema, waachie wanasiasa, ambao nao wanapaswa kufanya siasa safi zisizogawa jamii. “Tunalinda taifa letu kwa...

MAONO YA RAIS DKT. SAMIA YAMEIPAISHA SEKTA YA ANGA-MAJALIWA.

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yameiwezesha Tanzania kupiga hatua kubwa za kimaendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo ya Anga.   Amesema hayo leo Jumatatu (Aprili 28, 2025) wakati alipofungua Mkutano wa 73 wa Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege kwa Ukanda wa Afrika (ACI Afrika) unaofanyika kwenye Hotel ya Mount Meru.   Amesema kuwa moja ya eneo ambalo Rais Dkt. Samia ameendelea kusimamia ni ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege nchini ikiwemo ujenzi wa kiwanja kipya cha ndege cha msalato kilichopo jijini Dodoma.   Ameongeza kuwa Rais Dkt. Samia anaendelea na uboreshaji wa viwanja vingine vya kimkakati vya Kilimanjaro, Unguja, Pemba, Mwanza, Kigoma, Tabora, Shinyanga na Sumbawanga. “Pia tunaendeleza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Serengeti unaolenga kukuza utalii wa mazingira huku tukihifadhi mfumo ikolojia wa Serengeti”. Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali imewekeza katika ununuzi wa vifaa vya kisa...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

Matarajio ya Hali Mbaya ya Hewa kwa Siku Tano.

Image
 

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO KUANZIA SAA 3.00 USIKU WA LEO TAREHE: 27/04/2025.

Image
 

JOWUTA , THRDC WALAANI WANAHABARI KUKAMATWA NA KUPIGWA.

Image
CHAMA cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binaadamu nchini (THRDC) wamelaani kuanza kuibuka matukio ya waandishi wa habari na watangazaji kukamatwa na baadhi kupigwa na hata kuharibiwa vifaa vyao vya kazi na vyombo vya dola. Kauli ya kulaani imetolewa leo Aprili 25 mwaka huu na Mwenyekiti wa JOWUTA Mussa Juma mkoani Mbeya, wakati wa mafunzo kwa wanahabari kuhusu uandishi wa habari za uchaguzi, ulinzi na usalama kazini. Mafunzo hayo yamehusisha waandishi kutoka mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ambapo Juma amesema matukio ya kukamatwa, kupigwa na kuharibiwa vitendea kazi hayakubaliki katika nchi inayojinadi kuwa inazingatia misingi ya kidemokrasia. Juma amesema katika siku za karibuni, kumeanza kutokea matukio ya baadhi ya wanahabari kukamatwa na vyombo vya dola, kupigwa na wengine kuzuiwa kufanyakazi, jambo ambalo sio sahihi. Mwenyekiti huyo, amesema mahusiano mazuri baina ya vyombo vya dola na wanahabari, yalikuwa yameimarishwa ...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO KUANZIA SAA 3.00 USIKU WA LEO TAREHE: 26/04/2025.

Image
 

RAIS SAMIA ATOA MSAMAHA KWA WAFUNGWA 4,887 KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO.

Image
Katika kuadhimisha miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametumia mamlaka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1) (a)-(d) ya Katiba na kutoa msamaha kwa makundi mbalimbali ya wafungwa nchini. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, msamaha huo umewahusu wafungwa waliotimiza vigezo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kupunguziwa sehemu ya vifungo vyao, kuondolewa kabisa kifungo, au kubadilishiwa adhabu.  Jumla ya wafungwa 4,887 wamenufaika na msamaha huo, ambapo 42 kati yao wameachiliwa huru mara moja na wengine 4,845 wataendelea kutumikia sehemu iliyobaki ya vifungo vyao baada ya msamaha huo. Miongoni mwa waliopata msamaha ni: Wafungwa waliopunguziwa sehemu ya vifungo vyao. Wafungwa wagonjwa sugu walioko hatua ya mwisho ya ugonjwa. Wafungwa wa maisha waliobadilishiwa vifungo vyao kuwa miaka 30. Wafungwa waliokadiriwa kunyongwa waliobadilishiwa adhabu kuwa kifungo cha maisha. Wa...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO KUANZIA SAA 3.00 USIKU WA LEO TAREHE: 25/04/2025.

Image

WAZIRI MAVUNDE ATOA SIKU 21 TUME YA MADINI KUPITIA MFUMO WA BIASHARA YA MADINI NDANI YA UKUTA MIRERANI.

Image
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameielekeza Tume ya Madini kupitia upya mfumo wa biashara ya madini ndani ya ukuta wa Mirerani, Wilaya ya Simanjiro, ili kuja na pendekezo bora zaidi la namna ya usimamizi na uendeshaji wa biashara ya madini ya Tanzanite kwa lengo la kuongeza thamani ya madini hayo ya kipekee na kuongeza manufaa kwa taifa. Ameyasema hayo leo, Aprili 24, 2025, wakati wa kikao maalum na Viongozi wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania (*TAMIDA*) kilichofanyika jijini Dodoma kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali yanayohusu biashara ya madini nchini, kwa lengo la kuwawezesha wafanyabiashara hao. “Mkapitie kwa uwazi na uadilifu mkubwa ili kwa pamoja tuje na pendekezo la kuboresha biashara ya madini ya vito ya Tanzanite. Lakini kubwa zaidi ni mkakati wa kuongeza thamani ya madini yetu ya Tanzanite ambayo hayapatikani kwingine duniani isipokuwa hapa Tanzania. Nawapa siku 21 kuanzia leo (Aprili 24, 2025) hadi Mei 15, 2025, mje na ripoti kuhusu mfumo bora wa bi...

RC CHALAMILA AZINDUA UTOAJI WA MIKOPO YA 10% MANISPAA YA TEMEKE.

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, leo Aprili 24, 2025, amezindua rasmi utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.  Uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga, Jijini Dar es Salaam. Akihutubia katika hafla hiyo, Mhe. Chalamila amesema kuwa mikopo hiyo isiyokuwa na riba ni jitihada mahsusi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuwawezesha wananchi kiuchumi, hususan wakazi wa Wilaya ya Temeke. “Lazima mikopo hii irejeshwe kwa wakati ili na wengine wapate fursa ya kunufaika,” alisisitiza Chalamila. Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wananchi kuacha tabia ya kulaumu Serikali badala yake watumie changamoto kama daraja la mafanikio.  “Unakuta mtu anatoka Kigoma pembezoni, anakuja mjini, anauza madafu, kesho na keshokutwa anakuwa mfanyabiashara mkubwa. Lakini mzawa wa hapa Temeke kila siku analalamika Serikali,” alisema Chalamila. Katika hat...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO KUANZIA SAA 3.00 USIKU WA LEO TAREHE: 24/04/2025.

Image
 

MAKUSANYO YA MAPATO MAGU YAPAA, SHULE 24 MPYA ZAFUNGULIWA.

Image
Mwenyekiti wa Halmaahauri ya Wilaya ya Magu, Simon Mpandalume amesema katika kipindi cha miaka mitano Halmashauri hiyo imeongeza makusanyo ya mapato ya ndani kutoka Sh bilioni 2.4 hadi bilioni 5.2.  Mpandalume ameyasema hayo leo Alhamisi wakati wa mkutano wa baraza la madiwani ambao pamoja na mambo mengine amewapongeza madiwani, Mkurugenzi Mtendaji na watumishi wa halmashauri kwa ushirikiano ambao umewezesha kupandisha wigo wa makusanyo ya mapato ya ndani. Amesema katika kipindi cha miaka mitano Halmashauri ya Wilaya ya Magu imefungua shule mpya 24 kwa kutumia mapato ya ndani.  Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Magu, Joshua Nassari ametoa wito kwa viongozi wanaohusika na usimamizi wa miradi kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati ili miradi hiyo isaidie wananchi. Pia ametoa pongezi kwa wadau na wananchi wa Wilaya ya Magu kuridhia mchakato wa maombi ya kuligawa jimbo la Magu amesisitiza kuwa mchakato huo ukikamilika utachochea maendeleo katika Wilaya ya Magu.  Mkurugenzi...

MAWAKILI WA SERIKALI TOENI USHAURI UNAOZINGATIA MASLAHI YA TAIFA-Dkt Possi.

Image
Mawakili wa Serikali wametakiwa kutoa ushauri wa kisheria unaozingatia maslahi mapana ya Serikali na Taifa ili kuiwezesha Serikali kuokoa fedha zitakazosaidia kukuza uchumi kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo. Wito huo umetolewa na Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi tarehe 24 Aprili 2025 wakati akizungumza na Mawakili wapya wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali (OWMS) kwenye mafunzo elekezi yaliyotolewa kwa watumishi hao yaliyofanyika Kibaha mkoani Pwani. ​ Akizungumza na Mawakili hao kwa njia ya mtandao, Dkt. Possi amesisitiza kuwa Mawakili wa Serikali wana jukumu la kutunza siri wakati wote wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku katika uendeshaji wa mashauri ya Serikali ili kulinda maslahi ya Serikali na kuleta heshima ya taaluma ya sheria nchini katika kuhakikisha kuwa Serikali inapata haki yake katika kila shauri linalofunguliwa dhidi yake au linalofunguliwa na Serikali dhidi ya watu wasio na nia njema na Serikali. Dkt. Possi alieleza kuwa OWMS ina jukumu kubwa la kuend...

Shule ya Sekondari Kisutu wajivunia mafanikio kuongezeka kwa ufaulu ndani ya miaka mitatu.

Image
SHULE ya Sekondari ya wasichana Kisutu wajivunia mafanikio ya kitaaluma kwa kufanya vizuri katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo huku ufaulu wa wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita ukipanda mwaka hadi mwaka.  Hayo yalisemwa na Mkuu wa shule hiyo Chiku Jumanne Mhando  katika mahafali ya saba  ya kidato cha sita iliyofanyika katika shule hiyo iliyopo Dar es salaam, ambapo wahitimu  318 walitunukiwa vyeti vya kidato cha sita.  "Shule yetu ya Sekondari Kisutu tunajivunia ufaulu mwaka hadi mwaka, 2022 jumla ya watahiniwa walikuwa 262 waliofanya mtihani wa kuhitimu elimu ya kidato cha sita, watahiniwa 40 walipata daraja la kwanza, watahiniwa 135 walipata daraja la pili, watahiniwa 84 walipata daraja la tatu, watahiniwa watatu walipata daraja la nne na hakuwepo mtahiniwa aliyepata daraja sifuri mwaka 2023, jumla ya watahiniwa walikuwa 249 ambapo katika mtihani wa kuhitimu kidato cha sita uliofanyika mwezi Mei mwaka 2023, watahiniwa 68 walipata daraja la kwanza, wa...