Posts

Showing posts from February, 2025

Rais Samia ashiriki Tanzania Comedy Awards akiwataka wasanii kushirikiana na kupendana.

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ashiriki kwenye hafla ya utoaji tuzo za Wasanii wa Komedi Tanzania (Tanzania Comedy Awards) katika ukumbi wa The Super Dome, Masaki Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 22 Februari, 2023.

SHIGONGO AMPA HEKO RAIS SAMIA KWA UTENDAJI KAZI WAKE KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MINNE.

Image
 Na Mwandishi Wetu,Dar es salaam. MBUNGE wa Jimbo la Buchosa, Erick Shigongo amesema katika kipindi kifupi cha uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya mafaniko mengi hususani katika kukuza uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja. Shigongo ameyasema hayo Jijini Dar es salaam Februari 22,2025 wakati akizugumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa hususani katika Jimbo lake. Amesema kutokana na mafanikio hayo watanzania wanapaswa kutumia utajiri uliopo nchini kwa kuleta maendeleo huku wakimsaidia Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kukuza uchumi huo. “Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu imefanya mambo mengi ya kimaendeleo katika Jimbo la Buchosa pamoja na kukuza uchumi wa nchi na mtu mmoja”amesema Amefafanua kuwa ndani ya miaka mitatu kwa upande wa Jimbo la Buchosa limepokea sh.bilioni 62.5 kwa shughuli za maendeleo ambazo zimejenga vituo vipya vya afya vitano, sekondari zaidi ya nane, zahanati 21 na madarasa kadhaa. Aidha aliwataka Watanzania ku...

*BARRICK YACHANGIA SHILINGI TRILIONI 3.6 SERIKALINI KWA KIPINDI CHA MIAKA MINNE*

Image
Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Dhahabu ya Barrick imechangia kiasi cha shilingi trilioni 3.6 katika Mapato ya Serikali kupitia kodi, mrabaha, na tozo mbalimbali kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2020 hadi 2024. Hayo yameelezwa Februari 13, 2025 Jijini Dodoma na Meneja Mkaazi wa Kampuni hiyo hapa nchini Dkt. Melkiory Ngido mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakati akiwasilisha Maendeleo ya Kampuni Tanzu Baona ya Barrick Gold na Serikali ya Tanzania inayofamika kama Twiga Minerals. Dkt. Ngido ameelezea kuwa, kwa mujibu wa takwimu za miaka minne kuanzia mwaka 2020 hadi 2024, Kampuni Barrick imewekeza zaidi ya dola bilioni 4.24 (Tsh trilioni 11) katika shughuli zake ndani ya nchi, huku dola bilioni 1.5 (Tsh trilioni 3.6) zikilipwa serikalini kupitia kodi, mrabaha, na tozo mbalimbali. Amesema kuwa, Kampuni ya Barrick ilipochukua usimamizi wa shughuli zake nchini Tanzania mnano mwaka 2019, kampuni hiyo imeendelea kuwa mdau mkubwa wa uchumi kupitia uwekezaji, ajir...

WANUFAIKA MIKOPO ELIMU YA JUU REJESHENI IWANUFAISHE NA WENGINE”-RC CHALAMILA

Image
Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya bodi ya mikopo ya wanzafunzi wa elimu ya juu februari 17 mwaka huu ambapo Rais Dkt Samia anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila amewataka wadau mbalimbali kushiriki maadhimisho hayo pia amewataka wahitimu wa vyuo  walionufaika na mikopo inayotolewa na Bodi kufanya marejesho ili kutoa fursa kwa wanafunzi wengine kuweza kunufaika Akizungumza na waandishi wa habari Feb 13, 2025 ofisini kwake Ilala Boma-Jijini Dar es salaam RC Chalamila amesema bodi ya mikopo ya elimu ya juu inaadhimisha miongo miwili yaani miaka 20 tangu kuanzishwa kwake ikiwa imenufaisha zaidi ya wahitimu 830,000 kwa kuwapatia mkopo hivyo ni muhimu kwa wahitimu walio katika ajira rasmi na waliojiajiri kufanya marejesho Aidha RC Chalamila amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu imeongeza bajeti ya fedha kwenye bodi hiyo kutoka shilingi bilioni miatano sabini kwa mwaka wa fedha 2021-2022 hadi kufikia...

Neno la siku

Image
“ Tunapenda kwa sababu yeye alitupenda kwanza”

TANZANIA YAPOKEA UJUMBE WAFANYABIASHARA KUTOKA FALME YA SAUDI ARABIA

Image
 TANZANIA YAPOKEA UJUMBE WAFANYABIASHARA KUTOKA FALME YA SAUDI ARABIA Serikali ya Tanzania, ikiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, pamoja na viongozi wengine wa serikali, imefanya kikao muhimu na ujumbe kutoka Falme za Saudi Arabia, Lengo likiwa ni kujadili fursa za uwekezaji na kukuza ushirikiano kati ya nchi hizi mbili. Ujumbe huu wa wafanyabiashara toka chemba ya uwekezaji kutoka nchini Saudi Arabia unaongozwa na Naibu Waziri wa Uchumi na Mipango wa Falme za Saudi Arabia, Mhe. Albara Alaskandarani, na Ujumbe huu umejumuisha wafanyabiashara 30 kutoka sekta mbalimbali, ikiwemo Nishati, Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Viwanda, Biashara na Uchukuzi.  Katika kikao hicho, Mhe. Albara Alaskandarani alitoa pongezi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi za kukuza uchumi, na kuongeza kuwa hatua hii inatarajiwa kutoa suluhisho la kudumu kwa changamoto mbalimbali za kimaendeleo. Kwa upande wa Sekta ya Nishati uliwakilishwa na N...

NENO LA SIKU

“  Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye”

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

NENO LA SIKU

Image
“ Msifungiwe nira pamoja na watu wasioamini. Kwa maana pana uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?”

KIVUKO CHA MV KILINDONI CHASITISHA HUDUMA MAFIA.

Image
 Kivuko MV. KILINDONI kinachotoa huduma kati ya Mafia Wilayani Mafia na Nyamisati Wilayani Kibiti Mkoani Pwani kitasimama kutoa huduma katika eneo hilo kuanzia siku ya leo Tarehe 12 Februari, 2025 ili kupisha matengenezo pamoja na kufungwa injini mpya. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kitengo cha masoko na uhusiano TEMESA kivuko MV. KILINDONI kimewasili leo kikiwa na abiria pamoja na mizigo eneo la Nyamisati kikitokea Wilayani Mafia.  Kivuko hicho kinatarajiwa kupekekwa Mkoani Dar es Salaam ambako kitakuwa huko kwa muda wa wiki moja kikifanyiwa matengenezo hayo ili kukiongezea ufanisi kiweze kurejea kikiwa bora na salama kwa watumiaji.  Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA), unawaomba radhi abiria wote kutokana na usumbufu watakaoupata kutokana na kukosekana kwa huduma ya kivuko hicho.
Image
 BASHUNGWA APONGEZA POLISI KUPATIKANA WANAFUNZI WALIOTEKWA MWANZA. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Wazazi na Wananchi kwa kufanikisha Operesheni ya msako mkali na kuwapata Wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Blessing Medium iliyopo Mwanza waliotekwa na kupatikana wakiwa salama. Aidha, Bashungwa ametoa onyo kali kwa watu wote wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani na usalama na kueleza kuwa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Vyombo vya Usalama limejipanga na lina uwezo na weledi wa kukomesha na kupambana na vitendo vyote vya kiuhalifu. “Wahalifu msijaribu uwezo wa Polisi, tutawafikia popote”amesema Bashungwa Bashungwa amesema hayo leo tarehe 11 Februari 2025  mkoani Mwanza mara baada ya kufika katika Shule ya Msingi Blessing Medium, na Makao Makuu  ya Polisi Mkoa Mwanza na kuzungumza na Walimu na Wazazi pamoja na Askari na Maafisa waliofanikisha zoezi la...

UTABIRI WA HALI YA HEWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

RC CHALAMILA KUJA NA MWAROBAINI WA KUONGEZA UFAULU MKOANI DAR ES SALAAM.

Image
  Mkoa wa Dar es salaam kukutanisha wadau wa elimu na wazazi kutafuta mwarobaini wa ufaulu wa wanafunzi. Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila amesema ni muhimu kufanya utafiti wa kina na kuhakikisha wazazi wanashirikishwa ipasavyo kwenye kuinua ufaulu wa wanafunzi ili    ndoto za Rais Dkt Samia zitimie na fedha nyingi anazozitoa kuimarisha miundombinu ya elimu zitimize lengo husika badala ya kutazama sababu chache zinazotolewa na kuonekana kusababisha ufaulu kuwa hafifu. RC Chalamila akizungumza leo Feb 10, 2025 Wilayani Temeke Jijini Dar es salaam katika mkutano na wadau mbalimbali wa elimu amesema Serikali chini ya Rais Dkt Samia imekuwa ikiimarisha miundombinu ya elimu na mazingira ya kufundishia na kujifunzia hivyo ni muhimu kwa kila mdau wa elimu ikiwemo wazazi, viongozi pamoja wataalamu kujielekeza kwenye kusaidia watoto ili kuinua viwango vya ufaulu kwa wanafunzi. RC Chalamila amesema hivi karibuni Serikali Mkoani humo inatarajia kufanya mkutano utaka...

NENO LA SIKU

Image
 “ Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]  “

UTABIRI WA HALI YA HEWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

Tanzania inaendelea na dhamira ya kushiriki katika kutekeleza Ajenda ya Maendeleo ya Afrika 2063-Mhe Dkt Mpango

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Tanzania inaendelea na dhamira  ya kushiriki katika kutekeleza Ajenda ya Maendeleo ya Afrika 2063 kupitia uwekezaji wa kimkakati katika sekta mbalimbali kama vile Miundombinu ya Usafirishaji, Nishati, Kilimo, Viwanda, TEHAMA, Uhifadhi wa Mazingira pamoja na maendeleo ya Rasilimali watu.   Makamu wa Rais amesema hayo alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 42 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Bodi ya Juu ya Shirika la Maendeleo la Umoja wa Afrika (AUDA – NEPAD) uliyofanyika kwa njia ya Mtandao na kuongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambaye ni Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah El- Sisi.   Aidha Makamu wa Rais amesema ni muhimu nchi za Afrika kuimarisha vyanzo vya mapato vya ndani kwa kutumia vema rasilimali za nchi kama vile madini pamoja na kushirikiana na sekta binafsi ili kuweza kukabiliana na upungufu wa fedha za ufadhili wa mirad...

MAMBO MUHIMU KUHUSU USALAMA BARABARANI.

Image
 *MAMBO MUHIMU KUHUSU USALAMA BARABARANI* 1. *CHUKUA TAHADHARI DHIDI YA AJALI ZA BARABARANI* kwani: (a)Duniani kote ajali za barabarani zinaua watu 1,190,000 kila mwaka, na zinaacha wengine zaidi ya milioni 50 wakiwa majeruhi; (b)Ajali za barabarani ni chanzo nambari 12 cha vifo vyote ulimwenguni (c)Ajali za barabarani zinachangia 24.4 ya vifo vyote ulimwenguni. (d)Ajali za barabarani ni chanzo Na.1 cha vifo kwa watoto na vijana kati ya umri wa miaka 5-29. (e)Ajali za barabarani zinaacha yatima, wajane, wagane, na kuleta simanzi kubwa katika familia (f)Ajali za barabarani zinavunja ndoa, zinatenganisha familia. (g)Ajali za barabarani zinaleta au kuongeza  umasikini katika familia (h)Ajali za barabarani zinafifisha ndoto za watoto na vijana. (i)Ajali za barabarani ni chanzo cha ulemavu mwingi wa ukubwani duniani. (j)Maisha yako, viungo vyako havina spea; ukishakufa umekufa, ukishapoteza mguu, huwezi pata mguu mwingine kama uliokuwa nao awali.  2. *FUNGA MKANDA* Kufunga mka...

Huu hapa utabiri wa hali ya hewa wa saa 24 zijazo kutoka TMA.

Image
 
Image
 RC CHALAMILA ATANGAZA UUZAJI VIWANJA  MABWEPANDE-KINONDONI -Asema Serikali imeshapima viwanja zaidi ya 2274. -Awataka wale wote waliovamia na kujenga kulipia viwanja hivyo mara moja kwa kuwa wamepunguziwa bei. Kufuatia maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kutaka waliovamia na kujenga kwenye eneo linalomilikiwa na shirika la maendeleo Dar es Salaam (DDC) lililopo Mabwepande kuuziwa viwanja kwa gharama nafuu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila kwa kushirikiana na shirika hilo pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya kinondoni ametangaza rasmi rasmi kuanza  kuuza viwanja katika eneo hilo Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 8, 2025 eneo la Mabwepande akiwa ameambatana Katibu Tawala wa Mkoa Dkt Toba Nguvila, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, viongozi wa DDC pamoja na wataalamu wa ardhi kutoka Halmashauri ya manispaa ya Kinondoni RC Chalamila amesema eneo hilo lenye viwanja zaidi ya 2274 vyenye ukubwa tofauti tofauti am...

Watanzania kila mmoja awe mlinzi wa miundombinu ya anwani za makazi-Waziri Majaliwa

Image
 **WAZIRI MKUU MAJALIWA AWATAKA WANANCHI KUILINDA MIUNDOMBINU YA ANWANI ZA MAKAZI** Na Mwandishi Wetu. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) amewataka Wananchi kulinda miundombinu ya Anwani za Makazi, akisema kuwa Serikali imepata taarifa kwamba vibao vya Anwani za Makazi, vinavyoonesha mitaa na barabara, vinaondolewa na watu wasio waaminifu na kisha kuuzwa.  Mhe. Majaliwa aliyasema hayo leo, Februari 8, 2025, katika hafla ya Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Anwani za Makazi, iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete (JKCC). "Tunazo taarifa kwamba, Anwani za Makazi tulizoziandika kwenye nyumba zetu, vibao tulivyoviweka kuonesha mitaa na barabara Watanzania wasio waaminifu, wanang'oa na kwenda kuviuza. Watanzania, Serikali yetu imetumia gharama kubwa kutengeneza mifumo hii na kuweka kwenye mitaa yetu, ni muhimu kwetu kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii," alisisitiza Waziri Mkuu Majaliwa. Aidha, Waziri Mkuu...

KAULI YA WIZARA YA AFYA KUHUSU UPATIKANAJI WA DAWA ZA ARV.

Image
Image
UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO .