Posts

Showing posts from May, 2026

MD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE .

Image
Na Mwandishi Wetu, Korogwe, Tanga Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange ameeleza kutoridhishwa na kasi ya mkandarasi anayetekeleza mradi wa maboresho ya Kituo cha Kufua Umeme cha Hale kutokana na kuchelewa kukamilika kwa Mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2022. Bw. Twange ameyasema hayo leo Aprili 22, 2026 wakati wa ziara yake ya ukaguzi katika mradi wa Hale pamoja na mradi wa usafishaji wa bwawa la Mto Pangani iliyopo katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambapo amemtaka mkandarasi wa Mradi wa Hale kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuongeza wafanyakazi pamoja na muda wa kufanya kazi ili ukamilike kwa wakati. “Siridhishwi sana na mwenendo wake. Mkandarasi amewahi kuomba nyongeza ya muda mara mbili na nimepata taarifa kuwa yuko kwenye hatua za kuomba nyongeza nyingine ya tatu. Ndio maana nimekuja kuona kuna nini,” amesema Bw. Twange. Amesema mradi huo una maeneo saba ya utekelezaji ambapo maeneo mawili tayari yamekamilika huku mengine yakien...

BAKWATA IMETANGAZA SIKUKUU YA DDI EL ADH HAA MEI 27.

Image
BARAZA Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA)imetangaza sikukuu ya Idd ell adh haa mwaka huu kwa mujibu wa Kalenda ya Kislaam itakuwa Mei 27 mwaka huu. Akizungumza na Waandishi wa habari Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Baraza la Waislam Tanzania BAKWATA Al haji  Nuhu Jabiri Mruma amesema kuwa Sikukuu ya Idd mwaka huu itasaliwa Kitaifa Mkoa Dar es Salaam Mei 27 Siku ya Jumatano katika Msikiti wa Mfalume Mohamed 1V Makao Makuu ya BAKWATA wilayani Kinondoni.  KATIBU wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania BAKWATA Al haj Nuhu Jabiri Mruma amesema swala ya idd siku hiyo itasaliwa saa 1.30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Idd mara tu baada ya Swala.. Aidha amesema kwa niaba ya Mufti wa Tanzania Shekhe Dkt.Abubakari Bin Zuberi Bin Ally Mbwana aliwatakia Waislam wote Tanzania maandalizi mema ya siku ya Idd

POLISI DAR ES SALAAM WACHUNGUZA KIFO CHA MMILIKI WA KIWANDA CHA XIL LI

Image
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linaendelea kuchunguza tukio la kifo cha Bhaozang Ge (50), raia wa China na mmiliki wa kiwanda cha kuchakata chupa cha XIL LI, aliyefariki dunia baada ya kushambuliwa na walinzi binafsi wa kiwanda chake. Akizungumza kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea Mei 16, 2026 majira ya saa 8:00 usiku katika eneo la Mabibo, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam. Amesema upelelezi wa tukio hilo unaendelea ili kubaini chanzo cha tukio pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria wote waliohusika. Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili kusaidia upatikanaji wa taarifa zitakazosaidia uchunguzi huo.

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

TMA NA BRAC MAENDELEO TANZANIA WAJADILI MIKAKATI YA KUIMARISHA USAMBAZAJI NA MATUMIZI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA.

Image
Dodoma Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) pamoja na BRAC Maendeleo Tanzania wamejadili mikakati ya kuimarisha usambazaji na matumizi ya taarifa za hali ya hewa nchini, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa jamii kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Majadiliano hayo yalifanyika Mei 15, 2026 katika Makao Makuu ya TMA jijini Dodoma yakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a . Akizungumza wakati wa kikao hicho, Dkt. Chang’a alisema TMA inaendelea kuthamini ushirikiano na wadau mbalimbali katika kuboresha huduma za hali ya hewa na kuhakikisha taarifa zinawafikia wananchi kwa wakati na kwa ufanisi zaidi. Alisema kikao hicho kimefungua fursa kwa taasisi hizo mbili kujadiliana maeneo ya ushirikiano katika utoaji wa huduma za hali ya hewa, tahadhari za mapema pamoja na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Aidha, alisema TMA ipo katika mageuzi ya kid...

TANESCO YATAKIWA KUBUNI TEKNOLOJIA MPYA KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA

Image
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ameielekeza TANESCO kuendelea kufanya tafiti na kubuni teknolojia mpya zitakazorahisisha utoaji wa huduma kwa wateja nchini.  Amesema dunia inabadilika kwa kasi kubwa hivyo Shirika hilo linapaswa kuendana na mabadiliko ya teknolojia ili kuongeza ufanisi na kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa urahisi. Akifungua mkutano wa mwaka wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO unaofanyika mkoani Dodoma, Mhe. Salome amesema matumizi makubwa ya mifumo ya kidijitali pamoja na akili mnemba yatasaidia kuboresha mawasiliano na kupunguza changamoto zinazowakabili wananchi wanapohitaji huduma za umeme. Aidha, ameagiza kufanyika kwa maboresho katika manunuzi ya vifaa pamoja na kuongeza uwezo wa vituo vya huduma kwa wateja ili kupunguza ucheleweshaji wa huduma.  Amesema hatua hizo zitasaidia kuongeza ufanisi wa kiutendaji na kuweka tabasamu kwa wananchi wanaotegemea huduma za TANESCO kila siku. Mhe. Salome pia amesisitiza umuhimu wa ushiriki...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

HUDUMA YA APITHERAPY YAVUTIA VIONGOZI MAONESHO YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII BUNGENI

Image
Dodoma Huduma ya tiba asilia ya udungwaji wa nyuki maarufu kama Apitherapy imeendelea kuwa kivutio kikubwa katika banda la Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwenye maonesho ya Wizara ya Maliasili na Utalii yanayoendelea katika viunga vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma. Idadi kubwa ya viongozi wanaotembelea banda hilo wameonesha kuvutiwa na huduma hiyo kwa kupata elimu na ufafanuzi kuhusu matumizi ya sumu ya nyuki katika tiba mbalimbali za asili, huku baadhi yao wakiamua kupata huduma hiyo mara moja baada ya maelezo. Huduma hiyo ya tiba asilia hutumia sumu ya nyuki kwa lengo la kusaidia kuimarisha kinga ya mwili na kupunguza baadhi ya matatizo ya kiafya. Katika huduma hiyo, nyuki huwekwa kwenye maeneo maalum ya mwili ili kumdunga mhudumiwa, au hutumika bidhaa zilizochakatwa kitaalamu zenye sumu ya nyuki. Akizungumza katika maonesho hayo, Mhifadhi wa TFS na Afisa Nyuki kutoka Hifadhi ya Mazingira Asilia Vikindu, Brenda Mwakipesile, alisema huduma hiyo imeku...

DAS TEMEKE AZINDUA OFISI YA WILAYA YA KITANESCO YA MIKWAMBE.

Image
Katibu Tawala wa Wilaya  ya Temeke Bw. Kimeta Mpui amezindua Ofisi mpya ya Wilaya ya KITANESCO Mikwambe ikiwa ni mkakati wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wa kuendelea kuwahudumia na kusogeza huduma mbalimbali zinazotolewa na TANESCO karibu na wananchi. Akizungumza  Mei 16, 2026 wakati wa zoezi hilo  amesema uzinduzi wa ofisi hiyo  umelenga  kuboresha utoaji wa huduma  kwa wananchi kutokana na mahitaji ya msingi ya Nishati ya umeme kwa wananchi yanavyozidi kuongezeka kila kukicha. Ameeleza kuwa hatua hiyo inaakisi maboresho ya kiutendaji yanayolenga kuongeza ufanisi na kupunguza changamoto ya umbali kwa wananchi ambao hapo awali walilazimika kufuata huduma katika ofisi za Mkoa wa KITANESCO Kigamboni. Amesema TANESCO imefanya mabadiliko makubwa ili kuendana na ongezeko la mahitaji ya huduma ya umeme kutoka kwa  wananchi hivyo ameipongeza TANESCO kwa kuanzisha ofisi hiyo nakuwataka wafanyakazi kuendelea  kuimarisha utoaji wa huduma bora zaidi k...

KAMATI YA URATIBU YA MRADI WA SOFF YAKUTANA JIJINI DODOMA.

Image
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), walifanya kikao kazi cha tano cha Kamati ya Uratibu  wa Mradi wa SOFF (Systematic Observations Financing Facilit)  katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma. Kikao hicho kiliwakutanisha wataalamu muhimu ili kupitia maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa SOFF na kujadili vipaumbele vya kimkakati kwa mwaka 2026, vinavyolenga kuhakikisha ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za mradi. Majadiliano yalijikita katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mwaka 2026,  ufuatiliaji na tathmini ya mradi, pamoja na shughuli za mawasiliano na uhamasishaji zilizopangwa kwa mwaka 2026. Kamati pia ilipitia maamuzi na maelekezo kutoka kikao cha Tatu cha Kamati Tendaji ya Mradi wa SOFF kilihofanyika Aprili 2026. Wakizungumza katika ufunguzi, Wenyeviti wenza wa kamati hiyo, Dkt. Paschal Waniha kutoka TMA na Dkt.Abbas Kitogo kutoka UNDP, walisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana ki...

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA UMEME WA BILIONI 4.17 NYASA.

Image
Mwenge wa Uhuru 2026 umezindua mradi wa kusambaza umeme vijijini unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Kitongoji cha Ndecha Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 4.17, hatua inayotarajiwa kuongeza maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa eneo hilo. Akizindua mradi huo Mei 16, 2026, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu Wazo Michael Mwang’onda, alisema Serikali imeendelea kuhakikisha huduma ya umeme inawafikia wananchi wa vijijini kwa gharama nafuu ili kuboresha maisha yao. Mwang’onda aliwahamasisha wananchi kujitokeza kuunganishiwa umeme kwa gharama ya shilingi 27,000 pekee, akisema huduma hiyo sasa ipo karibu na wananchi tofauti na zamani ambapo gharama zilikuwa kubwa zaidi. “Tunataka wananchi wachangamkie fursa hii ya umeme wa shilingi 27,000 ili kila nyumba iweze kupata huduma ya nishati na kuchochea maendeleo,” alisema. Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Hamisi Mrope, alisema mradi w...

SERIKALI KUIMARISHA NISHATI YA UMEME WILAYANI KONDOA.

Image
Katika jitihada za kuendeleza ustawi wa wananchi na kuchochea uchumi wa maeneo ya vijijni na vitongojini, Serikali inaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme wilayani Kondoa kupitia mpango wa kusambaza umeme katika vitongoji vyote vya wilaya hiyo.  Mpaka sasa vitongoji 113 vina umeme huku kukiwa na mradi unaoendelea wa kupeleka umeme katika vitongoji 60. Hayo yameelezwa leo Mei 16, 2026 na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba wilayani Kondoa, Dodoma. Mhe. Salome ameeleza kwamba katika mradi wa umeme unaotekelezwa sasa wa kusambaza umeme katika vitongoji 60 zaidi ya shilingi billion 21 imetengwa kuhakikisha mradi huo unakamilika ambapo kukamilika kwake kutafanya  Kondoa kubakiwa na vitongoji 88 tu ambavyo havina umeme  vitakavyofikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2030. Pia Mhe Salome ameeleza kwamba Serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 752 kwa ajili ya  kuhakikisha wananchi ambao miradi ya...

TANESCO YAWATAKA WANANCHI KUTOFANYA SHUGHULI ZA KIUCHUMI KATIKA MIUNDOMBINU YA UMEME.

Image
Wananchi wa mtaa wa wazo kata ya Tegeta jijijini Dar es Salaam wametakiwa kutojihusisha na shughuli za kibiashara katika maeneo ya miundombinu ya umeme ili kuepuka madhara mbalimbali yanayoweza kuwapata ikiwemo kupoteza maisha au kupata ulemavu. Rai hiyo imetolewa  Mei 15, 2026 na Mhandisi wa  usafirishaji umeme Dar es salaam Philemon Tirukaizile kwa kushirikiana na Seikali ya Mtaa wa Wazo wakati wakitoa elimu kuhusu athari za kufanya shughuli au biashara kwenye miundombinu ya umeme hasa katika njia kubwa za kusafirisha umeme. Akizungumza na wananchi wa eneo hilo Mwenyekiti wa Mtaa huo  Bw. Medard Mashauri amewataka wananchi hao kuelewa kuwa eneo walilopo ni hatarishi na ni mali ya TANESCO  hivyo hakuna sababu ya serikali kutumia nguvu kuwaondoa wananchi akiwasisitiza kuondoka wenyewe kwa hiari. ‘’Ni vyema wananchi ambao wameingia kwenye eneo la TANESCO  kuondoka  kwa hiari yao kwani serikali imeamua kuanza kutoa elimu kuhusu athari za kufanya biashara kwen...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO.

Image
 

TAKUKURU KINONDONI YADHIBITI UPOTEVU WA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 563.

Image
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kinondoni imefanikiwa kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali yenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 563 kupitia ufuatiliaji wa ukusanyaji wa ushuru wa huduma (Service Levy). Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni, Elizabeth Mokiwa amesema mafanikio hayo yamepatikana katika kipindi cha Januari hadi Machi 2026 baada ya kubaini baadhi ya wafanyabiashara kutolipa ushuru wa huduma kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa. Amesema baada ya ufuatiliaji huo, wafanyabiashara husika walitakiwa kulipa madeni yao kupitia control namba za Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, ambapo jumla ya Shilingi 563,663,820.15 zililipwa kutoka kampuni mbalimbali. Katika kipindi hicho, TAKUKURU pia ilifuatilia miradi saba ya maendeleo katika sekta za afya na elimu ili kuhakikisha inatekelezwa kwa ubora na kwa kuzingatia matumizi sahihi ya fedha za Serikali. Aidha, wananchi 6,571 walifikishwa ...

MKURUGENZI MKUU REA ATOA WITO KWA WATUMISHI KUENDELEA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA WELEDI.

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewanasihi watumishi wa wakala kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kufuata miongozo ya utumishi wa umma kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni zilizopo. Ametoa rai hiyo Jijini Dodoma Mei 15, 2026 katika kikao kazi na watumishi wote wa Wakala ambapo amewanasihi kuimarisha usimamizi wa miradi na kuwa sehemu ya miradi sambamba na kuimarisha mawasiliano na viongozi wa Serikali maeneo ya mradi. “Tusirudi nyuma, tusilewe sifa tufikirie mambo makubwa zaidi. Tuwe wabunifu, tuchape kazi kwa weledi na ushirikiano na hii ndiyo nguzo itakayofanya tuendelee kusonga mbele,” amesema Mha. Saidy. Mha. Saidy amesema Wakala umejipanga kuhakikisha miradi yote ya kusambaza nishati vijijini inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakikana. Katika kikao kazi hicho, watumishi walipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha utendaji wa kazi, kukumbushana kuhusu miongozo mbalimbali ya utumishi wa umma pamoja na...

TBS YAJIVUNIA SAFARI YA MIAKA 50 YA KUCHOCHEA UBORA NA USALAMA.

Image
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) imesema inajivunia mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, hususan katika kusimamia ubora wa bidhaa na huduma pamoja na kulinda afya na usalama wa walaji nchini. Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya miaka 50 ya shirika hilo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TBS Dkt.Ashura Katunzi, alisema safari ya nusu karne imekuwa na mafanikio makubwa yaliyosaidia kuimarika kwa sekta ya viwanda na biashara nchini. Alisema TBS imeendelea kuboresha mifumo ya kazi ikiwemo miundombinu ya maabara, matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) pamoja na kuimarisha ushirikiano na taasisi za viwango za kimataifa. Aidha, alisema mafanikio hayo yameiwezesha Tanzania kuongeza ushindani wa bidhaa zake katika masoko ya kikanda na kimataifa huku yakichochea ukuaji wa uchumi. “TBS imekuwa mhimili muhimu katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazozalishwa na kuuzwa nchini zinazingatia viwango vinavyok...