RC CHALAMILA AWATAKA WENYEVITI NA WATENDAJI KATA NA MITAA DAR KUSIMAMIA ULINZI NA USALAMA.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es alaam Mhe Albert Chalamila amewataka wenyeviti wa Serikali za mitaa pamoja na watendaji wa Kata Mitaa Mkoani humo kusimamia ulinzi na usalama kwenye ngazi ya mitaa na kata ili kuhakikisha Mkoa huo unakua Salama bila uwepo wa matukio ya uvunjifu wa amani wakati wote. Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika kikao kazi na Wenyeviti, Watendaji wa Kata na mitaa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Diamomd Jubilee RC Chalamila amesema suala la ulinzi na usalama linapaswa kuanzia kwenye ngazi ya mitaa na kata hivyo amewataka viongozi hao wa mitaa kusimamia suala hilo kwani katika baadhi ya mitaa kumekua na matukio ya uvunjifu wa amani. RC Chalamila amewataka viongozi hao ngazi ya Mitaa na Kata kusaidia kutatua changamoto za wananchi na sio wao kuwa ni chanzo cha kuongeza changamoto kwa wananchi ambapo pia ametumia nafasi hiyo kuwataka wenyeviti na watendaji kutambua kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo waendelee kuhimiza wananchi kuanzia ngazi ya mtaa kushiriki ucha...