Posts

Showing posts from September, 2025

Serikali Kupitia Wizara ya Mawasiliano Yajipanga Kupanua na kuboresha Mawasiliano Vijijini.

Image
Na Fidea Masunga,Dar es Salaam. Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imesema imejipanga kuhakikisha kila Mtanzania, awe mjini au kijijini, anapata huduma bora na za uhakika za simu pamoja na usikivu mzuri wa redio. Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu wa wizara hiyo,  Salome Kessy , alisema hayo alipofungua mafunzo ya ndani kwa wataalamu wa Mradi wa Miundombinu ya Mawasiliano Vijijini yanayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 29 hadi Novemba 7, 2025. Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wa kiufundi katika usimamizi wa mitandao ya simu vijijini, uendeshaji wa miundombinu ya mawasiliano, pamoja na utatuzi wa changamoto zinazohusu huduma za simu na intaneti. Kwa mujibu wa Kessy, kufikia Juni 2025 Tanzania ilikuwa na zaidi ya  laini za simu milioni 92 , sawa na upenyo wa asilimia 136. Aidha, kulikuwa na  watumiaji wa intaneti milioni 54 , sawa na upenyo wa asilimia 79. Alisema huduma za intaneti ya kasi zimewafikia wananchi ...

NCHI YENYE MADINI YA KIPEKEE, KUWA NA WANANCHI MASIKINI NI AIBU-DOYO

Image
Mgombea urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, akiendelea na kampeni zake Kanda ya Ziwa, amefanya mikutano ya hadhara katika Jimbo la Sengerema, eneo la Stendi ya Zamani, na Kata ya Buseresere, Mkoa wa Geita. Katika hotuba yake, Mhe. Doyo aliwataka wananchi wa Kanda ya Ziwa kutafakari kwa kina juu ya sababu zinazowafanya kuendelea kukosa maendeleo licha ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kushika dola kwa zaidi ya miaka 60. Mhe. Doyo aliwaahidi wananchi kuwa endapo watampa ridhaa ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atahakikisha wakulima wanapata fursa ya kuuza mazao yao katika masoko yenye tija na faida, badala ya kulazimishwa kuuza katika masoko yanayowanyonya na kuendeleza umaskini.  “Wananchi, mkiniamini na kunipa kura Oktoba 29, nitasimamia na kuhakikisha wakulima wanapata bei nzuri na zenye motisha kwenye mazao yenu yote. Haiwezekani mtumie gharama kubwa katika kilimo chenu halafu mpangiwe bei, hizi ni mbinu za kuendeleza umaskini wenu ili CCM waendelee kuwa...

MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MANISPAA YA SUMBAWANGA, MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SH. BILIONI 335 YAZINDULIWA.

Image
Mwenge wa Uhuru umepokelewa rasmi katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ukitokea Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ambapo unakimbizwa umbali wa kilomita 88.7. Katika mbio hizo, Mwenge wa Uhuru umeweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali yenye thamani ya shilingi Bilioni 30.3, Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Soko la Mazao Kanondo, ujenzi wa barabara kiwango cha lami kupitia mradi wa TACTIC, huduma za afya katika Hospitali ya Manispaa ya Sumbawanga, shule mpya ya msingi Pwela iliyojengwa kwa mapato ya ndani, pamoja na ofisi ya Wakala wa Misitu Tanzania.  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Bw. Ismail Ali Usi, ameipongeza Manispaa ya Sumbawanga kwa utekelezaji wa miradi hiyo kwa viwango vya ubora vinavyowaletea wananchi maendeleo endelevu. Kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 ni "Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu." Manispaa ya Sumbawanga imesisitiza kuwa imeupokea Mwenge wa Uhuru kwa heshima kubw...

MAKAMU WA RAIS AHUTUBIA KIKAO CHA 80 CHA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA.

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Tanzania inalaani kuibuka upya kwa ukiukwaji wa sheria za kimataifa na kupelekea matumizi ya nguvu kama njia ya kutatua migogoro hali inayopelekea ukatili uliokithiri kwa binadamu hususani watoto, wanawake, wazee pamoja na wagonjwa katika maeneo ya migogoro.   Makamu wa Rais amesema hayo wakati akihutubia Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.  Amesema uwepo wa mitazamo ya kibeberu, ikiwa ni pamoja na ile ya kuichukulia Afrika kuwa sehemu ya uchukuaji rasilimali na uporaji wa ardhi, pamoja na uwepo wa makampuni ya kimataifa kuendelea kufanikiwa kutokana na unyonyaji wa mali asili za Afrika, huku wakisababisha au kuunga mkono migogoro inapaswa kumalizika sasa.   Makamu wa Rais amesema Tanzania inauchukulia msimamo wa upande mmoja na matumizi mabaya ya nguvu za kijeshi, pamoja na kushindwa kwa jumuiya ya k...

GCAP Yaitaka Serikali Kuchukua Hatua Madhubuti Kukabili Umasikini, Usawa na Changamoto za SDGs

Image
Na Fidea Masunga,Dar es salaam. Mtandao wa Kupambana na Umaskini (GCAP) Tanzania umeitaka Serikali kuchukua hatua za haraka na madhubuti kukabiliana na umasikini na ukosefu wa usawa nchini, ili kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi wote kwa usawa. Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya utekelezaji wa Malengo Endelevu ya Dunia (SDGs), Mratibu wa Taifa wa GCAP Tanzania, Martina M. Kabisama, alisema licha ya mafanikio yaliyopatikana katika sekta za elimu, afya na miundombinu, bado kuna changamoto kubwa zinazohitaji suluhisho la dharura. “Serikali isichukulie suala hili juu juu, bali ihakikishe sera na bajeti zinawalenga wananchi wote bila kubagua. Wapo wananchi wanaoendelea kusalia nyuma kutokana na umasikini, ukosefu wa usawa na athari za mabadiliko ya tabianchi,” alisema Kabisama. Kwa upande wake, Rosemary Mwaipopo kutoka Dayspring Foundation, ambaye pia ni mwanachama wa GCAP, alisisitiza umuhimu wa Serikali kuongeza uwekezaji katika mifumo ya ulin...

DOYO: MIAKA 64 YA UHURU, SHULE ZINAENDELEA KUKOSA MAJI, KAMA SERIKALI IMESHINDWA KUPELEKA MAJI CHOONI, ITAWEZA NINI?

Image
Kwimba, Mwanza. Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, akiwa wilayani Kwimba mkoani Mwanza, amewaeleza wananchi kuwa changamoto zinazowakabili wakazi wa Kanda ya Ziwa zinafanana katika maeneo mengi, ikiwemo matatizo ya maji, afya, ajira na barabara. Akitoa mfano, Mhe. Doyo alisema kuwa akiwa wilayani Maswa, kata ya Binza, alishuhudia shule ya msingi yenye vyoo vinavyokosa maji, hali inayosababisha baadhi ya watoto kupangusia kinyesi kwenye kuta za vyoo baada ya kujisaidia. Alisema hali hiyo ni tishio kubwa kwa usalama wa afya ya jamii. “Miaka 64 ya uhuru, kilometa tano tu kutoka mjini, shule inakosa maji; jambo hili ni hatari sana. Kama serikali ya chama tawala inashindwa kupeleka maji hata chooni, itaweza nini kwa wananchi?” alihoji Mhe. Doyo mbele ya wananchi wa Kwimba. Akiendelea kuzungumza, aliahidi kuwa iwapo wananchi watamchagua, serikali yake itahakikisha inalinda usalama wa afya za Watanzania na kizazi kijacho. Aidha, Doyo...

TARURA GEITA YAHUDUMIA KM. 564 MAENEO YA MADINI.

Image
Geita, Wakala ya Barabara za Vijijini ma Mijini (TARURA) Mkoa wa Geita inahudumia  mtandao wa barabara upatao Km. 7274  na kati ya hizo Km. 564 ya barabara zinazohudumia maeneo ya madini. Hayo yamebainishwa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Geita Mhandisi David Msechu wakati akiongea na waandishi wa habari katika Maonesho ya Nane ya Madini yanayoendelea Mkoani hapa. Amesema katika mtandao huo asilimia 60 ya barabara zinapitika  hivyo maonesho hayo licha ya kutoa elimu kwa umma,wanashiriki kikamilifu kuhakikisha wanaendeleza ukuaji wa uchumi pamoja na kuendeleza huduma za jamii kwa kuhudumia barabara zinazoelekea maeneo ya migodini. Aidha, Mhandisi Msechu amesema kwa mwaka wa fedha 2024/2025 na 2025/2026 wametenga kiasi cha shilingi milioni 580 kwa ajili ya kukamilisha Km. 210  zikiwemo barabara zinazoelekea migodini. Kwa upande mwingine Mhandisi Msechu amesema TARURA Geita wana Maabara ya kisasa ambayo inapima ubora wa vifaa vya ujenzi wa miundombinu ya barabara pamoja na ...

Mpango Azungumza na Mfuko wa Hasara na Maafa, Akisisitiza Changamoto za Nchi za Afrika.

Image
Na Mwandishi Wetu, New York Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Hasara na Maafa yatokanayo na Mabadiliko ya Tabianchi (Loss and Damage Fund), Ibrahima Diong, pembezoni mwa kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachoendelea jijini New York, Marekani. Mazungumzo hayo yalilenga kujadili changamoto na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa mataifa ya Afrika, ikiwemo Tanzania, pamoja na mikakati ya kuongeza ukusanyaji wa fedha ili kusaidia nchi zinazoendelea ambazo zinaendelea kuchukua hatua za kukabiliana na madhara hayo licha ya changamoto ya rasilimali fedha. Mfuko wa Hasara na Maafa kutokana na mabadiliko ya tabianchi (Loss and Damage Fund) uliundwa mahsusi kutoa msaada wa kifedha kwa nchi maskini na zinazoendelea ambazo zinakumbwa na athari za majanga kama mafuriko, ukame na kupanda kwa kina cha bahari, ambazo mara nyingi haziwezi kuzuiwa hata kwa hatua za kukabiliana na tab...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo.

Image
 

Biteko: Motisha kwa Wahandisi Ndiyo Nguvu ya Maendeleo ya Taifa.

Image
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amesema zaidi ya asilimia 70 ya ubunifu mpya wa kiteknolojia duniani unatokana na taaluma ya uhandisi, hivyo Serikali itaendelea kuwapa motisha wahandisi ili kuongeza kasi ya maendeleo ya Taifa. Dkt. Biteko aliyasema hayo  jijini Dar es Salaam, alipomwakilisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kufungua maadhimisho ya 22 ya Siku ya Wahandisi Tanzania, yaliyozinduliwa kwa kauli mbiu  “Wajibu wa Wahandisi kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.” Alifafanua kuwa zaidi ya asilimia 90 ya maendeleo ya viwanda duniani yanategemea huduma za wahandisi, hivyo ni taaluma isiyoweza kuepukika katika safari ya maendeleo ya taifa lolote. “Kwa niaba ya Serikali, naomba niwakumbushe kuwa Taifa linawategemea sana.Tunawategemea, tunawahitaji, naomba mjue Serikali itaendelea kuwategemea wakati wote mnapotekeleza majukumu yenu,” alisema Dkt. Biteko. Ameongeza kuwa motisha kwa wahandisi wanaoshiriki katika mirad...