Kardinali Robert Prevost, mzaliwa wa Chicago, Marekani, ametangazwa rasmi kuwa kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki duniani na atajulikana kwa jina la Papa Leo XIV. Papa Leo XIV mwenye umri wa miaka 69, alihudumu hadi hivi karibuni kama Mkuu wa Dicastery ya Maaskofu katika Vatican. Pamoja na kuwa raia wa Marekani, Papa huyu mpya pia ana uraia wa Peru, ambako amehudumu kwa muda mrefu katika shughuli za kichungaji. Akihutubia maelfu ya waumini waliokusanyika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro kwa mara yake ya kwanza kama Papa, alitoa ujumbe wa matumaini na amani: “Amani iwe nanyi nyote. Wapendwa, ndugu na kina dada, hii ni salamu ya kwanza ya ufufuko wa Kristo. Ningependa kutoa salamu ya amani iwafikie familia zenu, ninyi nyote, popote mlipo. Amani iwe nanyi.” Uchaguzi huu unafuatia kifo cha Papa Francis aliyefariki dunia Jumatatu ya Pasaka tarehe 21 Aprili akiwa na umri wa miaka 88. Mazishi yake yalifanyika Jumamosi tarehe 26 Aprili na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka kote duniani. M...