MWENGE WA UHURU KATAVI 2025: RC MRINDOKO ATOA WITO WA UMOJA NA USHIRIKI MKUBWA KWA WANANCHI.
Katavi,
Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 20
Septemba 2025, RC Mrindoko amesema kuwa Katavi itapokea Mwenge wa Uhuru tarehe 23 Septemba 2025 ukitokea mkoani Kigoma. Amefafanua kuwa mapokezi
yatafanyika katika kijiji cha lfumbula, Kata ya Mishamo, Tarafa ya Kabungu, Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.
"Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukimbizwa umbali wa
takribani kilomita 769 na utatembelea miradi 46 yenye thamani ya shilingi bilioni 10.25. Kati ya miradi hiyo, miradi 9 itawekewa mawe ya msingi, 25 itazinduliwa, 3 itafunguliwa,
8 itatembelewa na mradi mmoja utahusu ugawaji wa majiko
ya gesi," amesema Mkuu wa Mkoa.
Ameeleza kuwa Mwenge utakimbizwa kwa siku tano katika
halmashauri zote za mkoa, tarehe 23 Septemba 2025 Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika, tarehe 24 Septemba
2025 Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, tarehe 25 Septemba 2025 Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, tarehe
26 Septemba 2025 Halmashauri ya Wilaya ya Mlele, na tarehe 27 Septemba 2025 Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.
Amebainisha kuwa baada ya mbio hizo, tarehe 28 Septemba
2025 Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa kwa Mkoa wa Rukwa ili kuendelea na mbio zake kitaifa.

Comments
Post a Comment