RC CHALAMILA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA MIRADI MIKUBWA YA ELIMU TEMEKE.


Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amefanya ziara ya kutembelea miradi ya ujenzi wa shule mpya wilayani Temeke na kujiridhisha juu ya taarifa iliyowasilishwa na Halmashauri hiyo juu ya ujenzi wa miradi yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 70 ambayo ujenzi wake umeanza


Akizungumza akiwa katika mradi wa ujenzi ya shule ya Sekondari Mwembe bamia wilayani Temeke Jijini Dar es Salaam RC Chalamila amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia katika utekelezaji wa miradi ya elimu lengo ni kuhakikisha kila mtoto aliye kwenye umri wa kusoma anapata fursa hiyo


RC Chalamila amesema kuwa maamuzi yaliyochukuliwa na Halmashauri hiyo kujenga miradi kwa fedha za ndani zaidi ya shilingi bilioni 70 ni maamuzi magumu yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi huku akisisitiza suala la ujenzi wa miradi ya shule na hospitali kufanywa kwa mfumo wa ghorofa kutokana na ufinyu wa Ardhi 


Aidha akizungumza wakati akifanya majumuisho ya ziara hiyo Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amesema ujenzi unaofanyika ni fedha iliyotolewa na Rais inayotokana na watanzania pamoja na vyanzo vingine ambavyo Rais amekuwa akivitafuta akijitoa katika kuwahudumia na kuwatumikia watanzania


Hata hivyo ametumia ziara hiyo kuwakumbusha watanzania kujitokeza kushiriki uchaguzi mkuu kwa kushiriki kupiga kura Oktoba 29,2025 ili kuwezesha kupata viongozi watakaoiongoza Tanzania kwa miaka mingine mitano kwa njia za kidemokrasia


Naye Nasoro Sultani Matope ni mmoja wa wananchi wakazi wa Mwembebamia waliojitokeza wakati wa ziara hiyo ameipongeza Serikali chini ya Rais Dokta Samia kwa kuleta miradi hiyo ya shule ambayo inakwenda kumaliza changamoto ya watoto wao kusafiri umbali mrefu kwenda shule



Comments

Popular posts from this blog

RC CHALAMILA AWATAKA WENYEVITI NA WATENDAJI KATA NA MITAA DAR KUSIMAMIA ULINZI NA USALAMA.

MAHAFALI YA NANE SHULE YA AWALI NA MSINGI SAI YAFANA, WAZAZI WATAKIWA KULEA WATOTO KATIKA MISINGI YA MAADILI MEMA.