SEGEREA YAITIKA KWA DK. SAMIA BONNAH KAMOLI.
MAELFU ya vijana, wadau wa michezo na viongozi wamejitokeza kushiriki mbio za Jogging na Tamasha la IJA Festival Season -1, lenye lengo la kuhamasisha wananchi kuchagua Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Familia Suluhu y na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Ladiaus Kamoli.
Tamasha hilo limeongozww na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) , Mary Chatanda ambaye amewataka vijana hususan wanamichezo kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 mwaka huu kumpigia kura Rais Dk. Samia, ambaye ni mdau mkubwa wa michezo.
Chatanda , amesema Ilani ya CCM ineeleza wazi kuhusu kuboresha sekta ya michezo hususan, viwanja vya michezo ili michezo iwe ajira rasmi.
“CCM imeteua mgombea mzuri wa urais Dk. Samia, ambaye naye anapenda michezo. Oktoba 29 kila mmoja aende kupiga kwani kura ni haki yako ya msingi kuchagua kiongozi wako kwa maendeleo,”amesema Chatanda.
Aidha amewataka vijana kuto kutishwa na uzushi wa Oktoba 29 kuwepo kwa maandamano.
“Msiogope, watu wanaosema kuna maandamano. Kwa ni nani anaye watisha vijana. Anaweza kuwatishia nyau?Uchaguzi upo na hawaitaiweza serikali ya CCM” ameeleza.
Ameongeza Rais Dk. Samia ndiye amiri jeshi mkuu hivyo hakuna atakaye furukuta kuingia barabarani.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Nasra Mohammed, aliwataka vijana wa mkoa huo kujitokeza kumpa kura za heshima Rais Dk. Samia.
Naye Mgombea Ubunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah, amewataka vijana hususan wana michezo kuhakikisha Oktoba 29 wanampigia kura Dk. Samia, yeye na madiwani wote wa CCM katika Jimbo hilo.





Comments
Post a Comment