RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI WAPYA IKULU NA BALOZI.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wapya ambapo amemteua Bw. Tido Mhando kuwa Mshauri wa Rais wa Habari na Mawasiliano
Huku Bw. Bakari Steven Machumu akichukua nafasi ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Bi. Sharifa Bakari Nyanga aliyepewa majukumu mengine.
Aidha, Bw. Lazaro Samuel Nyalandu ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania.


Comments
Post a Comment